'Nimegandisha mayai yangu kwa sababu sijapata mpenzi'

Chanzo cha picha, HANDOUT
- Author, Amy Walker, Philippa Roxby & Rozina Sini
- Nafasi, BBC
Idadi ya watoto waliozaliwa Uingereza na Wales, kwa sasa iko chini zaidi tangu miaka ya 1970, takwimu rasmi zinaonyesha.
Kiwango cha uzazi - hutazama ni watoto wangapi wanaozaliwa na kila mwanamke wakati wa miaka yake ya kuzaa – kwa sasa kiko chini zaidi katika rekodi.
Uingereza sio nchi pekee yenye tatizo hilo - nchi nyingi zinakabiliwa na kupungua kwa uzazi na zingine zinafanya juhudi kubwa kuongeza uzazi.
Nini kimesababisha kuanguka kwa uzazi? Kuna gharama kubwa ya kulea watoto, kufanya kazi na changamoto ya kupata mpenzi sahihi.
Lakini pia kuna ushahidi kwamba vijana wengi hawana mpango wa kuwa na watoto kabisa – nje ya sababu hizo.
BBC imezungumza na wanawake wawili na wanaume wawili wenye umri wa miaka thelathini - umri wa wastani ambapo kwa watu wa Uingereza na Wales wanakuwa wazazi - kupata mawazo yao juu ya suala hilo.